Nenda kwa yaliyomo

Ulaya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun[1]; inaitwa pia Uropa kutoka Kigiriki: "Ευρώπη", jina la mungu jike Europa) ni bara lililoko katika Kaskazini ya Dunia, likipakana na Bahari ya Aktiki upande wa kaskazini, Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi, na Bahari ya Mediterania upande wa kusini. Mpaka wake wa mashariki kwa kawaida hufafanuliwa kupitia Milima ya Ural, Mto Ural, Bahari ya Kaspi, Milima ya Kaukazi, na Bahari Nyeusi, ingawa mipaka hii ni ya kijiografia na kihistoria zaidi kuliko ya kisiasa. Kwa eneo la takriban kilomita za mraba milioni 10.18, Ulaya ni bara dogo la pili baada ya Australia lakini lina idadi kubwa ya watu, ikifikia zaidi ya milioni 750, na hivyo kuwa moja ya maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu duniani.

Ulaya ina historia ndefu na imechangia pakubwa katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, na kitamaduni duniani. Bara hili lina mataifa 44 yanayotambulika kimataifa, yakiwemo mataifa makubwa kama Ujerumani, Ufaransa, na Uingereza, pamoja na madola madogo kama Vatikani na Liechtenstein. Umoja wa Ulaya (EU) ni moja ya miungano muhimu ya kisiasa na kiuchumi katika bara hili, ukiwa na wanachama 27. Aidha, Ulaya imekuwa kitovu cha mapinduzi mbalimbali, kuanzia Mapinduzi ya Kitaaluma na ya Viwanda hadi maendeleo ya demokrasia ya kisasa, na imeendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika masuala ya kimataifa.

Ramani


Ulaya kutoka angani.
Ulaya duniani.
Lugha za Ulaya.
Kanda za kiutamaduni za Ulaya kadiri ya Ständiger Ausschuss für geographische Namen (StAGN) ya Ujerumani.
Ulaya mwaka 1000 hivi.

Utawala

Katika karne ya 20, baada ya vita kuu mbili, nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali:

Kanda za Ulaya

Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa (UN categorisations/map). Lakini utaratibu huo haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati. Wajerumani, Waaustria, Waswisi, Wacheki, Waslovakia na Wapoland hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki ila Ulaya ya Kati. Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado, kwa mfano suala la Hungaria au Latvia.

Orodha ya Nchi na Maeneo ya Ulaya

Orodha ya Nchi na Maeneo ya Ulaya
Bendera Nchi/Maeneo Eneo (km²) Idadi ya Watu Mji Mkuu Jiji Kubwa Lugha Rasmi
Albania 28,748 2,829,741 Tirana Tirana Kialbania
Andorra 468 79,034 Andorra la Vella Andorra la Vella Kihispania
Armenia 29,743 2,767,923 Yerevan Yerevan Kiarmenia
Austria 83,879 9,006,398 Vienna Vienna Kijerumani
Azebajani (zaidi ni Asia) 86,600 10,353,269 Baku Baku Kiazabajani
Aislandi 103,000 366,425 Reykjavik Reykjavik Kiaislandi
Ayalandi 70,273 4,994,724 Dublin Dublin Kiingereza, Kigaeli
Belarusi 207,600 9,349,645 Minsk Minsk Kibelarusi, Kirusi
Bulgaria 110,993 6,447,710 Sofia Sofia Kibulgaria
Bosnia na Herzegovina 51,197 3,276,000 Sarajevo Sarajevo Kiserbia, Kikroeshia, Kibosnia
Estonia 45,227 1,331,796 Tallinn Tallinn Kiestonia
Hungaria 93,028 9,606,259 Budapest Budapest Kihungaria
Italia 301,340 60,317,116 Rome Rome Kiitalia
Jojia (zaidi ni Asia) 69,700 3,688,600 Tbilisi Tbilisi Kijojia
Korasia 56,594 3,850,695 Zagreb Zagreb Kikorasia
Kosovo 10,887 1,798,188 Pristina Pristina Kikosovo
Kupro 9,251 1,244,188 Nicosia Nicosia Kigiriki, Kituruki
Latvia 64,589 1,882,000 Riga Riga Kilatvia
Liechtenstein 160 39,315 Vaduz Schaan Kijerumani
Lithuania 65,300 2,794,000 Vilnius Vilnius Kilithuania
Luxembourg 2,586 634,814 Luxembourg City Luxembourg City Kifaransa, Kijerumani, Kiluxembourg
Malta 316 514,564 Valletta Birkirkara Kimalta, Kiingereza
Moldova 33,846 2,603,000 Chisinau Chisinau Kimoldova
Monako 2.02 39,511 Monaco Monaco Kifaransa
Norwei 385,207 5,391,369 Oslo Oslo Kinorwei
Poland 312,696 38,265,017 Warsaw Warsaw Kipolandi
San Marino 61 33,600 San Marino San Marino Kiitalia
Ubelgiji 30,689 11,584,008 Brussels Antwerp Kiholanzi, Kifaransa, Kijerumani
Ucheki 78,866 10,686,269 Prague Prague Kicheki
Udeni 42,925 5,932,654 Copenhagen Copenhagen Kideni
Ufaransa 551,695 68,042,591 Paris Paris Kifaransa
Ufini 338,424 5,541,037 Helsinki Helsinki Kifini, Kiswidi
Ufalme wa Muungano 243,610 67,736,802 London London Kiingereza
Ugiriki 131,957 10,724,599 Athens Athens Kigiriki
Uhispania 505,990 47,450,795 Madrid Madrid Kihispania
Uholanzi 41,543 17,407,585 Amsterdam Rotterdam Kiholanzi
Ujerumani 357,022 83,190,556 Berlin Berlin Kijerumani
Ureno 92,090 10,295,909 Lisbon Lisbon Kireno
Urusi (Sehemu ya Ulaya) 17,098,242 146,599,183 Moscow Moscow Kirusi
Vatikani 0.49 825 Vatican City Vatican City Kilatini, Kiitalia

Tanbihi

1. Kanda zinazotajwa (Ulaya ya Kusini – magharibi n.k.) zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisations/map. Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine (Asia, Afrika, au Oceania). Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti; pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao.

2. Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia; namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee.

3–5. Guernsey, Kisiwa cha Man, and Jersey ni maeneo ya kujitegemea chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza.

6. Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira, ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika.

7. Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika, wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani ya Moroko, Afrika ya Kaskazini.

8. Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini, Bahari Hindi au Oceania.

9. Uholanzi: Idadi ya wakazi ni ya 2004; Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali.

10. Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki

11. Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

12. Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus.

13. Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

14. Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul.

15. Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

Tazama pia

Marejeo

  1. Hivyo asili ya neno "Ulaya" ni sawa na "wilaya"; Krapf 1882 Swahili-English dictionary anaeleza: ""ULAYA (WALAYA au WILAYA ya) ... mother-country in contradistinction to colonies, foreign possessions or parts"; Sacleux 1939 Dictionnaire Swahili-Francais anataja kama etimolojia ya Ulaya "Ar. Hind. ولاية wilaya, pays etranger" (=nchi ya kigeni); Madan 1903 "Wilaya, n. (1) native land, home, but commonly used of foreigners, and so (2) Europe. Ulaya Uzungu, Europe. U, Hindi, India. Ulaya wa Wareno, Portugal